Tuesday, August 18, 2015

ATCL yaanza safari za Mwanza



SHIRIKA la ndege la taifa (ATCL) limerejesha safari zake kuelekea mkoani Mwanza ikiwa ni sehemu ya mpango wa shirika hilo kupanua huduma kwa wateja wake hapa nchini.
Safari ya kwanza ya shirika hilo kuelekea mkoani Mwanza ilifanyika mwishoni mwa juma lilopita kwa kukutumia ndege yake aina ya CRJ- 200, baada ya safari hizo kusimama tangu mwezi Agosti mwaka mwaka jana.


Akizungumza na waandishi wa habari mara tu baada ya kuwasili kwa ndege hiyo Uwanja wa ndege wa Mwanza, Kaimu Afisa Uhusiano wa Shirika hilo, Bi Lily Fungamtama alisema uamuzi wa kurejesha safari hizo umezingatia mahitaji ya wateja wa shirika hilo.
“Tumepokea maombi mengi kutoka kwa wateja wetu wakiwemo wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao kwa kuhusisha majiji haya mawili. Kwa kuwa ATCL ni shirika mama la ndege hapa nchini tukafanya kila jitihada kuhakikisha tunarejesha safari zetu kuelekea jijini Mwanza,’’ 
alibainisha Fungamtama huku akiongeza kuwa shirika hilo litafanya safari zake mara mbili kwa siku katika siku zote saba za wiki.

Alisema ili kukabiliana na ushindani wa kibiashara dhidi ya mashirika mengine ya ndege yanayofanya safari zake kuelekea mkoani humo, shirika hilo limewekeza zaidi kwenye ubora wa huduma zake sambamba na kutoa huduma zake kwa gharama nafuu.

No comments:

Post a Comment