ASKARI Magereza wa Gereza
la Mbigili Wilayani Kilosa
wakimwomba mkuu wa jeshi hilo nchini, Kamishina John Minja kuwatembelea ghafla na kuzungumza nao katika gereza hilo
ili wamweleze bayana ufujwaji fedha na rasilimali za umma unaofanywa na mkuu wa
gereza hilo.
Wakizungumza na mwandishi wa habari
hizi kwa sharti la kutotajwa majina yao,baadhi ya asikari katika gereza hilo
wakimtaja mkuu huyo SSP.Charles Kimbi walisema tangu aingie kuongoza gereza
hilo Mwaka jana amekuwa akifuja mali za umma kwa manufaa yake sambamba na
kuwanyanyasa asikari hao kinyume na taratibu za utumishi ndani ya jeshi
hilo.
Hata hivyo alipotafutwa kutoa
ufafanuzi wa madai yanyomkabili mbali na kushindwa kukili au kukataa, alimtaka
mwandishi wa habari hizi kumtajia waliomfikishia taarifa hizo na kumtaka
maswali hayo kuwasiliana na Kamishina Minja au mkuu wa magereza mkoa RPO Kato
Ruginnura.
Baadhi ya mambo ambayo amekuwa
akiyafanya kwa manufaa take kwa muijibu wasikari hao ni pamoja na Kukodisha
ardhi ya serikali kwa shilingi 50,000 kwa ekari Mpunga na Mahindi huku akipiga
marufuku kwa mtumishi kulima katika eneo hilo zaidi ya eka moja.
Kwa mujibu wa asikari hao mkuu huyo
wa gereza SSP Kimbi amejimilikisha mradi wa klabu'Bwalo' ulioanzishwa na
asikari hao kwa ajili ya kusogeza huduma ya vinywaji na burudani mbalimbali
huku akiwalazimisha kuendelea kuchangia gharama za uendeshaji ikiwemo Umeme na
kulipia king'amuzi cha DSTV.
Aidha walisema Kigogo huyo amefuta
utaratibu wa asikari kupewa siku sita nje ya siku 28 za sheria kwa ajili ya
mamatizo ya njiani aendapo likizo na kurudi sambamba na kupiga marufuku
watumishi hao kufyatua tofari za kuchoma kwa ajili ya kujiandalia makazi baada
ya kustaafu.
Katika ufafanuzi wake Mkuu wa
magereza Mkoa RPO Kato Ruginnura mbali na kushindwa kutoa ufafanuzi wa taasisi
hiyo kuruhusu ukodishwaji maeneo yake na fedha zinazokusanywa kwa wakodishwaji
na walishaji mifugo kutofahamika ziendako alikili jeshi kutoa siku sita kwa
upendeleo hasa kwa asikari wa mikoa ya mbali na kituo.
Alisema kuhusu Mabwalo yaliyo kwenye
magereza nchin kote ni sehemu ya utawala kwakua lengo ni kumwezesha
asikari kambini na familia zao kuwa na sehemu ya kupumzika hasa baada ya
kazi za siku.
No comments:
Post a Comment