![]() |
Juma Kaseja akionesha jezi yenye jina lake kwa wanahabari |
KIPA
wa
zamani wa Simba Juma Kaseja amsaini mkataba wa kujiunga na klabu ya Mbeya City Agosti
19, 2015 mbele ya meneja wake mpya Athumani Tippo na kumaliza maswali ya kuwa
angecheza wapi msimu ujao.
Taarifa hizi huenda ni pigo kwa
kocha wa Mwadui FC ya Shinyanga, Jamhuri Kihwelu ambaye alikiri katika vyombo
vya habari kuwa anahitaji huduma ya Kaseja kikosini mwake.
Kabla ya kusaini mkataba na Mbeya City, Juma Kaseja alikuwa nje ya uwanja kwa
kipindi cha zaidi ya miezi nane baada ya kuingia katika mgogoro wa kimkataba na
iliyokuwa klabu yake ya Yanga na kufanya kesi hiyo kutinga mahakamani.
No comments:
Post a Comment