Saturday, August 22, 2015

MRADI wa biogesi waanza kazi nchini Kenya


Mtambo wa Gesi Nakuru, nchini Kenya

MRADI  mkubwa wa kuzalisha nishati kwa kutumia biogesi au gesi viumbe umeanza kufanya kazi kusini magharibi mwa Kenya, miaka mitatu baada ya ujenzi wake kuanza.

Mradi huo wa kwanza kabisa wa aina yake barani Afrika umejengwa mjini Nakuru na una uwezo wa kuzalisha megawati 2.6 za umeme na utaunganishwa na gridi ya taifa na kufanya gharama ya umeme zishuke zaidi.
 Mradi huo wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 7.5, utapunguza gharama ya serikali inayotokana na manunuzi ya mafuta kwa ajili ya kuendesha mitambo ya kuzalisha umeme
. Gavana wa Kaunti ya Nakuru Kinuthia Mbugua amesema mradi huo utapunguza uchafuzi wa mazingira na kuokoa gharama za kununua lita milioni tano za diseli ambazo hutumika kuzalisha kiwango cha umeme kama huo kila mwaka.

No comments:

Post a Comment