WAUMINI wa kanisa la kiinjili la Kilutheli Tanzania KKKT dayosisi
ya Morogoro wanakusudia kuiburuza mahakamani Halmashauri kuu ya Dayosisi hiyo
na Asikofu wake kwa kukiuka katiba ya dayosisi hiyo na kumpitisha kwa nguvu
asikofu Jacob Ole Mameo kukuendelea kuwaongoza.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na
kutoa barua ya tarehe 11/Julai kumbu namba KAM/2015/01 tunayo kwenda kwa mkuu
wa KKKTnchini Asikofu Dr.Alex Malasusa na nukuu ya katiba inayoliongoza kanisa
hilo Dayosisi ya Morogoro katika chaguzi,baadhi yao Gabriel Nzalayaimisi,
Robert Mwanga na Maiko Loweza walisema kilichofanyika katika kura ile ni
'magumasdhi' ya kulindana.
" katika ufafanuzi wake
msharika huyo alisema waliamua kumwandikia barua asikofu mkuu Dk. Malasusa
kuomba ufafanuzi juu ya yaliyotokea lakini amewapuuza na sasa wanasubiri hadi
Agosti 9 kwa mujibu wa siku 28 waliotoa kwa kiongozi huyo na halmashauri kuu
hiyo ya dayosisi nakuwa kama hakutakuwa na la ziada watakwenda mahakamani.
katika ufafanuzi wao washarika hao
walisema kura zilipopigwa kwa mara ya kwanza mbele ya asikofu mkuuDk. Malasusa,
Asikofu anayelalamikiwwa Jacob Mameo alipata kura 98 hapana 68 kati ya kura
zaidi ya 113 alizopaswa kupata.
walisema kura hizo zilipopigwa kwa
mara ya pili na hata kwa mara ya tatu asikofu Mameo alipata kura 97 huku 71
zikimkataa jambo ambalo kwa mujibu wa katiba ya Dayosisi hiyo 2011 kufungu(vi)C
kuchagua viongozi kipengele (2) hapaswi kuendelea na nafasi hiyo.
Alipotafutwa katibu wa dayosisi hiyo
Mchungaji Mathias Mduma kutoa ufafanuzi wa kikatiba baada ya kukosekana
ofisini,alikili kulitambua suala hilo ingawa hakuwa tayari kulitolea maelezo
kutokana na siku nzima jana kuhitajika mahakamani.
hata hivyo asikofu Jacob Mameo
hakutaka kuzungumzia suala hilo kutokana na suala kuwa kikatiba zaidi huku
akimshauri mwandishi kuwasiliana na kati wake kwakua ndie anayeelewa na anaweza
kutoa tafsiri njema.
No comments:
Post a Comment