![]() |
| Msikiti wa Aqsa uliopo Jeresalem |
TAASISI ya Al-Azhar ya Misri imetahadharisha kuhusu matokeo mabaya ya
uvamizi wa mara kwa mara wa Wazayuni dhidi ya Msikiti wa Al-Aqsa.
Al-Azhar imetoa
tahadhari hiyo juu ya taathira za suala hilo zitakazoamsha
ghadhabu na hasira ndani ya nyoyo za Waislamu wanaoishi ndani na nje ya ardhi
tukufu ya Quds.
Taasisi ya Al-Azhar ya
Misri imetahadharisha kuhusu matokeo mabaya ya uvamizi wa mara kwa mara wa
Wazayuni dhidi ya Msikiti wa Al-Aqsa. Al-Azhar imetoa indhari juu ya taathira
za suala hilo zitakazoamsha ghadhabu na hasira ndani ya nyoyo za Waislamu wanaoishi
ndani na nje ya ardhi tukufu ya Quds.
Taarifa iliyotolewa na Al-Azhar imelaani wito uliotolewa kwa walowezi wa
Kizayuni wa kuuvamia msikiti wa Al-Aqsa pamoja na mipango ya kuiyahudisha Quds
tukufu na kufuta utambulisho wake wa Kiislamu.
Al-Azhar imezitaka nchi zote wapenda amani kuchukua hatua haraka iwezekanavyo ili kuzuia uchokozi na uvamizi wa kinyama wa utawala wa Kizayuni dhidi ya Quds tukufu na njama zake za mtawalia za kuliyahudisha eneo hilo. Taarifa hiyo aidha imesisitiza kwamba kadhia ya Palestina itaendelea kubaki ndani ya nyoyo na fikra za Waislamu.
Jumuiya za walowezi wa Kizayuni ziitwazo "Hekalu la Kadhai" zimetoa wito kwa magenge ya walowezi hao kuchukua hatua ya kuuvamia msikiti mtukufu wa Al-Aqsa kuanzia Jumapili ya leo. Hatua hiyo imechukuliwa sambamba na kuanza sherehe za kile kinachoitwa "Sikukuu ya Mwanga" zitakazoendelea hadi siku ya Alkhamisi
Al-Azhar imezitaka nchi zote wapenda amani kuchukua hatua haraka iwezekanavyo ili kuzuia uchokozi na uvamizi wa kinyama wa utawala wa Kizayuni dhidi ya Quds tukufu na njama zake za mtawalia za kuliyahudisha eneo hilo. Taarifa hiyo aidha imesisitiza kwamba kadhia ya Palestina itaendelea kubaki ndani ya nyoyo na fikra za Waislamu.
Jumuiya za walowezi wa Kizayuni ziitwazo "Hekalu la Kadhai" zimetoa wito kwa magenge ya walowezi hao kuchukua hatua ya kuuvamia msikiti mtukufu wa Al-Aqsa kuanzia Jumapili ya leo. Hatua hiyo imechukuliwa sambamba na kuanza sherehe za kile kinachoitwa "Sikukuu ya Mwanga" zitakazoendelea hadi siku ya Alkhamisi

No comments:
Post a Comment