Wednesday, December 2, 2015

CCM wilaya ya Kilombero wampongeza Rais Magufuli

CHAMA cha mapinduzi CCM wilayani Kilombero kimempongeza Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk.John Magufuli kwa kasi aliyoanza nayo na kuahidi kumuunga mkono kwa juhudi hizo.


Aidha alimpongeza Rais Dk.Magufuli kwa umakini wake uliomwezesha kumpata na kumteua Majaliwa Kasimu Majaliwa kuwa waziri mkuu wa serikali ya awamu ya tano nchini.

Hayo yalisemwa na wenyekiti wa ccm wilayani humo Abdallah Kambangwa wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake na kuahidi kumuunga mkono wakati wote awapo madarakani.

Katika mazungumzo hayo Kambangwa alisema hotuba ya ufunguzi wa Bunge mjini Dodoma iliakisi maneno na ahadia alizokuwa akizisema wakati wa kampeni na kuongezwa nguvu na utekelezwaji ahadi hizo anaoufanya sasa.

Amewataka watanzania kumuunga mkono kwa uteuzi wake na kumpa ushirikiano yeye pamoja na wateule wake katika kutekeleza kauli mbiu ya serikali ya awamu ya tano ya hapa kazi tu.

Akielezea malengo yao baada ya uchaguzi ambapo chama hicho kimepoteza majimbo mawili ya Kilombero na Mlimba,Kambangwa alisema kuna baadhi ya wanachama walikihujumu chama na wao watakaa na kuwajadili kisha kuwachukulia hatua.

Hata hivyo alisema kwa sasa uchaguzu umemalizika na watu wafanye kazi na kuwata wananchi waondoe tofauti zao za itikadi na waijenge Kilombero mpya na wao kama chama watahakikisha wanaisimamia serikali katika kuarakisha maamuzi na kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji.





No comments:

Post a Comment