Wednesday, December 2, 2015

MKUU wa mkoa wa Morogoro apiga marufuku biashara holela

Mkuu wa mkoa wa Morogoror Dk Rajabu Rutengwe 
SERIKALI  mkoani Morogoro imepiga marufuku biashara holela  za matunda,mbogambaoga,juisi na aina zote za vyakula katika maeneo ya mikusanyiko ya watu zikiwemo stendi za mabasi kuunga mkono agizo la Rais Dk.John Magofuli kuweka miji safi na kutokomeza maambukizi ya ugonjwa wa Kipindupindu.


 Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa mkoa Morogoro Dk.Rajabu Rutengwe wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juu ya azima ya mkoa kuunga mkono tamko la Rais kufuta maadhimisho ya siku ya uhuru 9 Desemba badala yake kufanya usafi katika miji nchini.

“mwaka huu inatimia miaka 54 ya Uhuru wa Taifa letu, jukumu letu ni kutekeleza agizo la Rais Dk.Magufuli na mpango kazi wetu ni kufanya usafi kuondoa maambukizi ya Kipindu pindu kilichoripotiwa kwa mara ya kwanza tarehe 18/8/2015 Manispaa ya Morogoro baadae wilayani Gairo,Kilombero,Mvomero na Ulanga”alisema Dk.Rutengwe.

No comments:

Post a Comment