Tangazo
hilo amelitoa kwenye mkutano mkuu wa ushirikiano kati ya Uchina na nchi za bara
Afrika, ambao umeanza leo jijini Johannesburg. Viongozi kadha wa mataifa ya
Afrika wanahudhuria.
Tangazo
la fedha hizo za mabilioni ya dola ambazo zitatolewa kupitia ruzuku, mikopo na
ufadhili wa miradi ya maendeleo lilisubiriwa, lakini kiasi cha fedha
kilichoahidiwa kimezidi matarajio, mwandishi wa BBC aliyeko Afrika Kusini Karen
Allen anasema.
Sehemu
kubwa ya usaidizi huu wa kifedha sana utatolewa kupitia miradi ya miundo mbinu,
kusaidia kusisimua ukuaji wa kiuchumi, lakini maelezo zaidi hayajatolewa.
Kiongozi
mwenza wa mkutano huo Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amesifu ushirikiano kati
ya Uchina na nchi za Afrika.
Amesema
watu wanaoishi Uchina na Afrika ni theluthi moja ya watu wote duniani, na
kwamba hilo ni soko kubwa la bidhaa.
Uchina,
nchi yenye uchumi wa pili kwa ukubwa duniani.

No comments:
Post a Comment