Saturday, December 5, 2015

CWT manispaa ya Morogoroyamwaga vifaa vya ujenzi kwa walimu

MKUU wa idara ya jinsia walimu wanawake CWT taifa Mwandile Kiguhe akiwaasa walimu 17 waliostaafu ualimu Manispaa ya Morogoro.

CHAMA cha walimu CWT manispaa ya Morogoro kimeendeleza mpango wake wa kumwaga vifaa mbalimbali vikiwemo vya ujenzi na samani vyenye zaidi ya shilingi Mil.7,340,000 kwa walimu wastaafu sambamba na kuboresha mazigira ya kufundishia mashuleni.


Katika hafla fupi ofisi ya chama hicho mkoani humo,Katibu wa Manispaa Raphael Munada alisema mbali na baraza la cwt taifa kupendekeza walimum wasitaafu kupata bati kamati tendaji ya wilaya hiyo ilipendekeza mifuko ya saruji ili walimu hao wakaboreshe makazi yao.

"baraza liliazimia kila mwalimu mwanachama apate bati zenye thamani yashilingi 340,000 lakini kamati tendaji imepitisha walimu wetu wastaafu 17 wapate mifuko 25 ya saruji kil mmoja yenye thamani ya shilingi 350,000...pia kuboresha maeneo ya kazi kwa kutoa samani vikiwemo viti vya kisasa na plastiki"alifafanua Munada.  

Mgerasimi mkuu wa idara ya jinsia walimu wanawake CWT taifa Mwandile Kiguhe kwa niaba ya ya Makmu wa Rais wa chama hicho alisema mbali na kuwa sehemu ya kuangana na walimu wanachama wastaafu ila imeboreshwa na kuwa haki yao baada ya kuboreshwa katiba katika kifungu cha 6.2(d) toleo la sita 2014.

"niwaase! kustaafu sio mwanzo wa kuvunja na kukiuka haiba na maadili ya utumishio wa ualimu,tunajua zipo changamoto nyingi zinawakabili ikiwemo la mazoea ya utumishi lakini pia athari za kisikolojia na uchumi...kikubwa mkaendelee kuwa mfano ulaiani"alifafanua Mwandile.

Aidha alisema kustaafu kwa utumishi sio mwisho wa kupta huduma katika chama hicho ispokuwa huduma zitaendele kwao kwakua kwa mubu wa katiba upo uananachama wa aina yingi ukiwemo wa ushiriki na ule wa kawaida.


No comments:

Post a Comment