Monday, December 28, 2015

JAPAN na KOREA Kusini zafikia makubaliano

Waziri wa kigeni wa Japan Fumio Kishida (kushoto) asalimiana na mwenzake wa Korea Kusini Yun Byung-se
JAPAN na Korea Kusini zimefikia makubaliano ya kihistoria kuhusu wanawake waliolazimishwa kuhudumu katika madanguro kama watumwa wa ngono wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia.

Mzozo huo umeathiri uhusiano kati ya mataifa hayo mawili, Korea Kusini ikitaka kuombwa msamaha “kwa dhati” na kutolewa kwa fidia kwa waathiriwa.
Mwafaka wa sasa ndio wa kwanza kuhusu suala hilo tangu 1965 na umepatikana baada ya pande zote mbili kuahidi kuharakisha mazungumzo.
Tangazo hilo limetolewa baada ya waziri wa mashauri ya kigeni wa Japan Fumio Kishida kuwasili Seoul kwa mashauriano na mwenzake Yun Byung-se.
Baada ya mkutano Kishida aliambia wanahabari kwamba Waziri Mkuu Shinzo Abe ameomba msamaha kutoka kwa “wote walioathirika”.
Wanawake takriban 200,000 walilazimishwa kuwa watumwa wa ngono kwa wanajeshi wa Japan wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya DUnia, wengi wao wakitoka Korea.


No comments:

Post a Comment