Monday, December 28, 2015

MIMBA nyingi nchini Uingereza hutungwa siku ya krismas

TAKWIMU  kuhusu watoto wanaozaliwa Uingereza umebaini mimba nyingi hutungwa wakati wa Krismasi kuliko wakati mwingine wowote ule wa mwaka.

Takwimu hizo za kipindi cha miongo miwili kutoka Idara ya Taifa ya Takwimu zinaonyesha watoto wanaozaliwa huongezeka sana wiki 40 (miezi 9) baada ya msimu wa sikukuu.
Hili huenda linatokana na wanandoa kutumia muda mwingi pamoja wakisherehekea, au kulenga makusudi mwanzo wa mwaka mpya wa shule ambao huanza mapema Septemba nchini humo.
“Ongezeko la watoto wanaozaliwa mwishoni mwa Septemba ni ishara kwamba mimba nyingi hutungwa wiki chache kabla ya Krismasi na kuendelea hadi siku chache baada ya Krismasi kuliko wakati mwingine wowote wa mwaka,” idara hiyo imesema


No comments:

Post a Comment