Monday, January 4, 2016

OPERESHENI ondoa mifugo kuanza wilayani Kilombero

SERIKALI wilayani Kilombero imetangaza tena kuendesha operesheni ondoa mifugo yote iliyoibuka na kuingia kwa kasi na kutishia kuangamiza asili ya bonde la Kilombero.


Tamko hilo limetolewa tarafani Mngeta na mkuu wa wilayaya Kilombero, mkoani Morogoro  Lephy Gembe wakati akizindua nyumba ya kulala wageni ya Sahani Lodge mali ya Sahani Masanja aliyeamua kupunguza mifugo na kujenga nyumba ya biashara ya kulala wageni .

Dc.Gembe alisema uamuzi huo unakuja kufuatia kuibuka ongezeko kubwa la wahamiaji katika bonde hilo ya marufuku iliyotolewa na serilikali mwaka 2012.

"tumekaa na kamati za ulinzi na usalama za wilaya Kilombero na Ulanga mwishoni mwa wiki na kufanya ukaguzi kwa ndege ambapo tumejionea uharibifu mkubwa unafanyika katika bonde hilo dhiidi ya mifugo iliyoingia kwa wingi...tumekubaliana kufanya oparesheni"

Kwa mujibu wa Dc huyo kwa upande wa wilaya ya Kilombero mifugo mingi imefichwa katika maeneo yasiyofikika kwa urahisi kata ya Chisano huku upande wa wilaya mpya ya Malinyi maeneo mengi yaliyotengwa kama ardhi oevu yamevamiwa na vigogo kwa kilimo kikubwa.

Amewataka wafugaji wavamizi na wakulima wanaolima katika eneo la ardhioevu kutoka haraka katika bonde hilo kabla ya kuondolewa kwa nguvu na kutoa rai kuwa serikali haitomwogopa mtu wakati wa zoezi hilo.

Akimzungumzia mfugaji Sahani Masanja ambaye ameamua kupunguza mifugo yake na kuanzisha nyumba ya kulala wageni,Gembe alisema wafugaji wengine wanatakiwa kuiga mfano wa mwenzao kwani hivi sasa atakuwa na biashara ya kudumu hivyo kuwa na uhakika wa kusomesha watoto wake na kufanya masuala yake ya maendeleo.


No comments:

Post a Comment