Wednesday, January 13, 2016

UFARANSA yapiga marufuku baadhi ya Taasisi za kiislamu nchini humo

Waziri wa mambo ya ndani nchini Ufaransa Bernard Cazeneuve
SERIKALI  serikali nchini Ufaransa  imepiga marufuku Taasisi kadhaa za utamaduni zinazomilikiwa na msikiti mmoja ndani ya nchi hiyo.

Waziri wa Mambo ya Ndani nchini Ufaransa Bernard Cazeneuve, amesema  hayo mapema  leo baada ya kumalizika kikao cha Baraza la Mawaziri na kuongeza kuwa, taasisi hizo za Kiislamu zinamilikiwa na msikiti wa Lagny katika viunga vya mji wa Île-de-France nchini humo.
Aidha Waziri huyo wa Mambo ya Ndani wa Ufaransa amedai kuwa, viongozi wa Taasisi hizo walikuwa wakichochea vitendo vya kigaidi nchini Ufaransa.


No comments:

Post a Comment