Wednesday, January 13, 2016

NAKALA za bajeti nchini Nigeria zapotea

 NAKALA za bajeti rasmi ya serikali ya Nigeria ya mwaka wa 2016, zimetoweka kutoka bunge la nchi.

 kwa mujibu wa mbunge mmoja aliyezungumza na wanahabari   ambaye hakutaka jina lake litajwe.alisema Bunge la Senate lilishindwa kuanza kujadili mapendekezo ya bajeti hiyo kwa sababu ya nyaraka hizo kupotea.
Hali hiyo sasa huenda ikahujumu uchumi wa Taifa hilo ambao umeathirika pakubwa kutokana na kushuka kwa bei ya mafuta.
Rais Muhammadu Buhari aliwasilisha nyaraka hizo kwa mabunge yote mawili mwezi uliopita.
Serikali ya nchi hiyo ilikuwa imependekeza nyogesa ya asilimia ishirini ya matumizi ya serikali, na kuifadhili nyongesa hiyo kupitia mikopo zaidi huku bei ya mafuta ikiendelea kushuka.





No comments:

Post a Comment