Monday, January 25, 2016

MOCHUWARI hospitali ya Morogoro yazidiwa


Hospitali ya mkoa wa Morogoro
HALI ya chumba cha kuhifadhia marehemu Hospitali ya rufaa mkoani Morogoro ni mbaya.


Mbiu ya maendeleo Media  imetembelea chumba hicho na kushuhudia miili ya binadamu ikiwa imetapakaa sakafuni na kudondosha maji yenye harufu mbaya hali inayotishia hata watumishi wa chumba hicho kushindwa kufanya kazi kwa ustadi.

Baadhi ya ndugu,jamaa na marafiki wakisubiri kuchukua miili ya jamaa zao wakizungumza kwa masikitiko kwa nyakati tofauti nje ya ya eneo hilo,waliitupia lawama serikali kwa kushindwa kutenga bajeti ya kutosha kuboresha na kuongeza majokofu yaliyokatika chumba hicho ili kichukue miili mingi kwa muda mfupi.

“Hii siyo haki kwa nduguzetu kuwatelekeza chini na kuwacha wakiharibika,ukweli hali hii ni mbaya kama unavyoona ukweli inatisha maana marehemu wameachwa chini wanaharibika kama hawana jamii ya kuwasaidi kuwa katika hali salama…serikali itafute uwezekano wa kuboresha hii ni nyumba maalumu ambayo kila mtu ataipitia”alisema Mohamed Kipande wa Mwembesongo.

Walisema tatizo hilo limekuwa likijitokeza mara kwa mara kutokana na serikali kupuuza kuongeza na kuyafanyia matengenezo ya mara kwa mara majokofu yanyotumika kuhifadhia miili hiyo.


“tatizo la chumba hiki ni serikali kuto kijali kwa kukifanyia matengenezo ya mara kwa mara ndio maana kinafanya kazi kwa kubahatisha,leo ndugu zetu wana adhilika kama hawana ndugu tunaitaka serikali ilitatue tatizo hili mapema na itenge fedha za ukarabati kila baada ya miezi mitatu…kumbuka kunaongezeko kubwa la marehemu kutokana na ongezeko la watu mkoani hapa”alisema Filimedia Kusaga.

No comments:

Post a Comment