Tuesday, March 22, 2016

SERIKALI yaombwa kupunguza kodi mzigo kwa wakulima

SERIKALI nchini Tanzania imeombwa kupunguza kodi ya mazao ili kuwawezesha wakulima kukabiliana na changamoto za kiuchumi zinazowakabili.

Hayo yamebainishwa hivi karibuni na Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania,bwana  Jarson Kalile wakati akiongea na wanahabari jijini Dar es salaam.
Bwana Kalile amesema kodi zilizo mzigo kwa wakulima ni pamoja na ushuru wa halmashauri ya wilaya asilimia tano ya bei ya mkulima, ushuru wa utafiti asilimia 0.75 ya bei ya mnadani, mfuko wa maendeleo ya kahawa uliaonzishwa na wadau asilimia 0.5 ya bei ya mkulima, ada ya leseni ya kuuza kahawa nje zinazotozwa na Bodi ya Kahawa (TCB).
Aidha Mwenyekiti huyo amezitaja  ada za maghala, leseni, leseni ya kiwanda cha kukoboa kahawa, ada ya kibali cha kuuza kahawa nje kwa njia ya mauzo ya moja kwa moja pasipo kupitia mnadani na kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwenye vifaa mbalimbali vya kuhudumia kahawa yakiwamo magunia kuwa ni kikwazo cha maendeleo ya mkulima .




No comments:

Post a Comment