Tuesday, March 22, 2016

JOTO kuongezeka katika miji ya Mombasa na Dar es salaam ,Afrika mashariki

Makao makuu ya mamlaka ya hali ya hewa Duniani
SHIRIKA hirika la Hali ya Hewa Duniani limetahadharisha  wasiwasi wake kutokana na kuongezeka joto katika sayari ya dunia,eneo la Pwani ya Afrika mashariki.

 Katika kipindi cha siku chache zilizopita, wataalamu wa hali ya hewa nchini Kenya na Tanzania wameonya kuhusu kiwango cha joto kali katika miji ya Mombasa na Dar es Salaam na wakaazi wa miji hiyo wametakiwa kuchukua hatua za kuzuia vifo vitokanavyo na joto kali.
 Imetabiriwa kuwa miji hiyo inaweza kupata kiwango cha joto la nyuzi 36 au zaidi katika siku chache zijazo.

Shirika la Hali ya Hewa Duniani, WMO limesema kiwango cha joto kupindukia cha mwaka 2015 ni moja ya viashiria hivyo.
WMO imedokeza viashiria vingine kuwa ni mafuriko na ukame kupindukia, hali ya joto isiyotabirika, kuongezeka kwa joto la maji ya bahari na kupungua kwa kiwango cha barafu.
WMO imesema tayari miezi ya Januari na Februari mwaka huu imekuwa na viwango vya juu vya joto huku barafu kwenye bahari ya Artic ikipungua na kuyeyuka kwa kasi isiyo ya kawaida.
Akifafanua zaidi kuhusu hali inavyotabiriwa baadaye katika mazungumzo na waandishi wa habari huko Geneva, Uswisi, Mkurugenzi mkuu wa WMO Petteri Taalas amesema katika karne zijazo kiwango cha maji ya bahari kitaongezeka kwa mita moja zaidi kama joto litaongezeka kwa nyuzi joto mbili.

Amesema iwapo hatua hazitochukuliwa katika kupunguza hewa chafuzi basi tutashuhudia kiwango cha maji ya bahari kikiongezeka kwa mita tano ifikapo mwaka 2500.

No comments:

Post a Comment