Mbunge wa Morogoro Mjini Abdul Aziz Abood(kati) |
HATIMAE
mbunge wa Morogoro mjini AbdulAzizi
Abood amekabidhi matundu 10 ya vyoo vya kisasa yaliyogharimu shingi 7,500,000
yakiwemo mawili ya walimu katika shule ya msingi Mkwajuni kata ya Kichangani
pia kukagua ukarabati wa barabara za lami unaoendelea mjini humo kwa gharama ya
shilingi Mil.536.5.
Kujengwa na kukabidhiwa kwa matundu
hayo kati ya 24 yanayohitajika shuleni hapo kunatokana na uzembe wa uongozi wa
kata na shule hiyo kuliosababisa kukosa vyoo kwa wanafunzi na walimu kwa muda
mrefu hivyo wakaguzi wa shule kutishia kuifunga.
Akikabidhi matundu hayo kwa
mkurugenzi wa manispaa hiyo Theresia Mahongo, mbunge Abood alisema ameamua kuinusuru
shule na kifungo hicho akitumia fedha zake za mfukoni ili kuwaepusha wazazi na
kero ya kufukuzana na migambo wa manispaa kusaka michango bila kujali ukata
unaowakabili.
Awali kabla ya makabidhiano hayo
kuliibuka malumbano ya kisiasa bada ya mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na
mendeleo Chadema katani humo Abdalah Kumburu kumshukuru mbunge huyo kwa
kurejesha fedha za mfuko wa jimbo kwa wanachi hao kupitia ujenzi huo.
"nimpongeze mbunge wetu kwa
uwajibikaji wake na moyo wake wa dhati kutumia fedha za mfuko wa jimbo kuokoa
janazi la shule kufungwa tunataka wabunge wa namana hii na yeye tunamsihi
aendelee hivyohivyo"alisema Kumburu.
Kauli hiyo ilimlazimu Abood kusimama
na kusema" jamani tuache malumbano yasiyo na hoja ili kupotosha
wanachi,fedha zilizotumika ni kutoka mfukoni mwangu na kama hamuamini njooni
ofisini niwaonyeshe mapato na matumizi ya fedha za jimbo"
Kwa upande wake mkaguzi wa shule
aliyetaka kuifunga shule hiyo Mwalimu Victoria Bengesi alisema waliamua shule
ifungwe baada kujiridhisha kuwa mazingira ya wanafunzi na walimu
kufundishia,kusoma na kujifunzia hayakuwa mazuri.
No comments:
Post a Comment