Wednesday, March 4, 2015

HALMASHAURI Kilombero yanunua Greda kukabiliana na tatizo miundo mbinu


Afisa manunuzi wa H/W Kilombero Dinawi Gabriel akipewa funguo ya Greda
HALMASHAURI ya wilaya ya Kilombero imenunua greda jipya kwa shilingi mil.493 ili kukabili tatizo la ubovu wa barabara zake sambamba na kukuza uchumi wake kwa kulikodisha.


Katika makabidhiano ya greda hilo kwa niaba ya mkurugezi Mtendaji wa halmashauri hiyo,Afisa manunuzi wa halmashauri hiyo Dinawi Gabriel alisema kufika kwa greda hiyo kutaongeza mapato ya ndani ya halmashauri na pia kupunguza gharama za halmashauri.

Dinawi alisema ununuzi wa greda hilo ni utekelezaji wa maagizo ya baraza la madiwani la halmashauri hiyo ambayo waliagiza kununuliwa greda kwa ajili ya kuchonga barabara za halmashauri sambamba na Roller kwa ajili ya kushindilia barabara hizo.

Alisema kwa sasa wamepata greda na mwishoni mwa mwezi huu wanategemea kupokea Roller na wametenga shilingi milioni 230 kwa ajili ya ununuzi wa kifaa hicho pamoja na gharama za usajili na usafirishaji.

Afisa huyo wa manunuzi alisema kuwa greda hilo limefika wakati muafaka kwani wakandarasi wengi wanaopewa kazi katika wilaya hiyo wanakosa vifaa vya ujenzi ikiwemo greda na kwa sasa itarahisisha utendaji wao wa kazi kwa kulilodi greda hilo.
Akielezea utaratibu wa kutengeneza barabara za vijiji,Dinawi alisema wahusika watatoa gharama ndogo za utendaji ikiwemo mafuta na malipo kwa opereta huku pia wanaruhusu wilaya jirani kukodisha greda hilo.
Hata hivyo Dinawi alisema kwa kipindi kilichopita cha bajeti halmashauri ilipata kiasi cha shilingi bilioni 3 kwa ajili ya matengenezo ya barabara kutoka kwa wafadhili mbalimbali na shughuli zinaendelea ila wangekuwa na greda lao mapema gharama hizo zingepungua.
Kwa upande wake Mhandisi mauzo wa kampuni ya GF Trucks&Equipment Ltd ambao ndio walipewa tenda ya ununuzi Juma Hamsini alisema greda walilolileta ni aina ya Terex lililotengenezwa nchini Marekani.
Hamsini alisema wameamua kutoa kwa mkopo greda hilo kwa halmashauri hiyo tokana na halmashauri hiyo kuwa moja kati ya halmashauri zinazokuwa kwa kasi na ukuaji huo wa kasi unahitaji huduma za kijamii na miundombinu.
Mhandisi huyo alisema kampuni yao  ni ya wazawa na  inahusika na uuzaji wa mitambo ya ujenzi na majengo na wanatoa mikopo yenye masharti nafuu na haina riba kwa taasisi za serikali kwa miezi 12 na wamekwisha saidia zaidi ya halmashauri 60 toka mwaka 2007 na taasisi za serikali 10 kwa kukopesha magari na mitambo.
Alisema katika kuthibitisha kiwango cha ubora wanatoa garantii ya masaa 2000 au miaka 2 kwa mitambo na kilomita 20,000 au mwaka mmoja kwa magarimagari hivyo kutoa wito kwa watendaji kuwa mitambo wanayonunua isiwanufaishe wao bali itumike kwa kunufaisha halmashauri kwa kukodisha wadau mbalimbali

No comments:

Post a Comment