Wednesday, March 4, 2015

SHIRIKA la kirai nchini Burundi laitisha mgomo wa nchi nzima


Wafanyabiashara nchini Burundi
SHIRIKA la kiraia la kupambana na ufisadi na ughali wa bidhaa nchini Burundi limetishia kuitisha mgomo wa nchi nzima nchini humo.

Shirika hilo limemtishia Rais Pierre Nkurunziza kwamba, siku ya Alkhamisi litaitisha mgomo wa nchi nzima. Taarifa ya shirika hilo la kiraia imebainisha kwamba, litasubiri jibu la Rais Nkurunziza hadi hatua ya mwisho kabla ya kuitisha mgomo huo.
Uamuzi wa shirika hilo la kiraia umetokana na kuongezeka bei za bidhaa muhimu kama mafuta, kupanda kwa kodi za simu na mengineyo.
Serikali ya Burundi imenukuliwa ikitangaza juu ya kuweko juhudi za baraza la mawaziri la kulitafutia ufumbuzi tatizo hilo. Shirika la Kupambana na Ufisadi la Ughali wa Bidhaa nchini Burundi limeshamtumia barua mbili Rais Pieere Nkurunziza wa nchi hiyo likielezea wasi wasi wake kuhusiana na kuchelewa kutolewa majibu ya matakwa yao. Mkuu wa shirika hilo, Gabriel Rufyiri amesema kuwa, wamebainisha wazi kuhusiana na tatizo hilo na wanasubiri majibu kwa kiwango hicho hicho cha uwazi. Amesema, endapo serikali ya Rais Nkurunziza itashindwa kutoa majibu ya kueleweka hadi kumalizika muda walioutoa, basi watawataka wananchi wa Burundi wafanye mgomo wa siku nzima siku ya Al-Khamisi.



No comments:

Post a Comment