Wednesday, March 4, 2015

MAWAZIRI WA Utalii Afrika mashariki kukutana mwishoni mwa mwezi


MAWAZIRI wa Utalii wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), wanatarajia kukutana mwishoni mwa mwezi huu kujadili pamoja na mambo mengine, migogoro ya kimaslahi katika sekta ya utalii katika nchi zao.

Ajenda kubwa ya mkutano huo itahusu mgogoro kati ya Kenya na Tanzania kuhusu kuzuiliwa kwa magari ya kusafirisha watalii kuingia na kutoka katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, jijini Nairobi.
Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani na Kupinga Ujangili, Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Lazaro Nyalandu, amesema kuwa, wanatarajia kukutana Machi 20 jijini Arusha na kueleza kwamba, tofauti hizo zitajadiliwa na kupatiwa ufumbuzi wa kudumu. Waziri Nyalandu amesema kuwa, Tanzania haitakubali kupoteza maslahi ya Watanzania na taifa kwa ujumla. Amesema kama ninavyomnukuu: "kilichotokea awali kwa sasa hakiko tena, mahusiano yetu na Jamhuri ya Kenya ni mazuri, kwa sababu hiyo tumeafikiana na mawaziri wa nchi hizo kukutana ili kuangalia njia ya kumaliza  mvutano unaoshindaniwa katika eneo hilo. Mwisho wa kunukuu. Ikumbukwe kuwa, Desemba mwaka jana, serikali ya Kenya ilizuia magari yote ya Tanzania yanayosafirisha watalii kutoka na kuingia katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, hali ambayo imezua mikwaruzano kati ya Kenya



No comments:

Post a Comment