Wednesday, March 4, 2015

DIRA ya mazingira kusikika kupitia Redio jamii Kilosa


Msitu wa Hifadhi
Mhariri mkuu wa  Mbiu ya Maendeleo Media Group, Bi Salma Mlamila ameeleza kuwa kipindi cha Dira ya Mazingira sasa kinarushwa hewani kupitia Redio Jamii ya Kilosa, mkoani Morogoro.

Kipindi hicho kimeanza  kurushwa rasmi februari 16, mwaka huu katika kituo cha Radio Jamiii kinachomilikiwa na Halmashauri ya wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro.

Kwa takribani miezi mitatu kipindi hicho kitagusa sekta ya Misitu na kitakuwa kikizungumzia jitihada za wakala wa Huduma za  misitu nchini(TFS),  hususani wilayani Kilosa  katika kutunza, kusimamia na kuhifadhi misitu .
Kipindi hicho kitakuwa kikirushwa kila siku ya jumamosi saa tatu usiku.
  Bi Salma Mlamila amewataka wadau mbalimbali wa mazingira kukiunga mkono kipindi hicho kwa kushiriki kipindi hicho, ambacho  kitakuwa kikirushwa kila siku ya jumamosi saa tatu usiku.
Amefafanua   kuwa, makala za vipindi hivyo zitakuwa zikipatikana katika blog  ya Mbiu ya Maendeleo ambayo ni www.mbiuyamaendeleo.blogspot.com





No comments:

Post a Comment