Friday, September 2, 2016

WACHUUZI wandamana nchini Kenya wakipinga vibanda vyao kuharibiwa

Waandamanaji jijini Nairobi
MAMIA ya wachuuzi waliokasirika wamefanya maandamano katika barabara za eneo la Eastleigh jijini Nairobi ili kupinga kuvunjwa kwa vibanda vyao.

Usiku kucha maafisa wa polisi waliharibu vibanda vilivyojaa kandokando ya barabara ambapo huweka bidhaa zao zote.
Operesheni hiyo ya polisi inafuatia malalamishi kutoka kwa wamiliki wa maduka ambao wanasema kuwa wamekuwa wakizuia watu kuingia katika maduka hayo.(bbc Swahili )


No comments:

Post a Comment