Thursday, September 1, 2016

MKUU wa wa Morogoro aombwa kutatua changamoto za elimu kata ya mkuyuni

Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk Steven Kebwe
DIWANI kata ya Mbuyuni Manispaa ya Morogoro amemwangukia mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk Steven Kebwe akimwomba kumwongezea nguvu ya uharakishwaji utatuzi wa changamoto zinazo wakabili katani humo ikiwemo ya upungufu vyumba vya madarasa,kukosefu wa maji na matundu ya vyoo shule ya msingi Mbuyuni.



Mbele ya Mkuu huyo wa Mkoa wa Morogoro Dk.Kebwe na Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro,John Mgalula wakati jumuiya ya Bohora mkoani Morogoro wakikabidhi madawati 50 shuleni hapo, Diwani Msuya alisema sambamba na tatizo hilo kuisha bado kunachangamoto zinazo fifisha elimu.

Diwani huyo alisema tangu shule hiyo ianzishwe mwaka 1969 inakabiliwa na changamoto ya miundombinu mibovu kutokana na jamii wakiwemo wazazi kutokuwa na ari ya kujitolea kuboresha elimu na kusisitiza juhudi za kipekee zinahitajika toka serikalini kufanikisha lengo.

Afisa mtendaji wa Kata hiyo,Jeniffer Rashid katika taarifa yake kwa mkuu huyo shuleni hapo akifafanua baadhi ya mapungufu kuwaa ni kupungua nyumba za walimu 25,matundu ya vyoo17,maktaba,chumba cha ushauri nasaha,meza 18, viti 20 vya walimu na kabati 9.

Shule ya msingi Mbuyuni inawanafunzi 7322 huku ati yao 6771 wakiwa ni watoto wa awali walioandishwa mwaka huu na 551 wanafunzi kuanzia darasa la kwanza hadi darasa la saba.
















No comments:

Post a Comment