Saturday, May 31, 2014

BAADA ya kuweka mtambo wa kudhibiti udanganyifu unaofanywa na makampuni ya simu,serikali yaingiza bilioni6.8



SERIKALI imeingiza jumla ya shilingi bilioni 6.8 kwa kipindi cha mwaka 2013/3014 kutokana na kodi inayolipwa na  mitandao ya simu nchini  baada ya kuweka mtambo maalum wa kudhibiti udanganyifu uliokuwa ukifanywa na wamiliki wa mitandao ya simu wasiokuwa waaminifu.

Waziri mawasiliano, sayansi na teknolojia Profesa Makame Mbarawa amebainisha hayo mapema leo bungeni mjini Dodoma wakati akiwasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2014/2015.

Profesa Mbarawa amesema kuwa wizara kwa kushiorikiana na tume ya mawasiliano nchini(TCRA) imeunda kamati maalum ya ufuatiliaji ili kuendeleas kudhibiti na kuzuia hali hiyo isitokee sanajari na kuongeza pato la Taifa kupitia mitandao ya simu.  

No comments:

Post a Comment