WAKATI
tukielekea
katika maadhimisho ya siku ya mazingira duniani ,wananchi wa Mwanza wameitaka
Serikali na wadau mazingira nchini kuandaa vipindi vya elimu kwa umma kupitia
redio na luninga ili kukabiliana na changamoto zinazoikabili tasnia hiyo.
Wakiongea na waandishi wa habari leo
asubuhi mjini Mwanza , baadhi ya wavuvi wa ziwa Victoria wamesema, bado elimu
ya mazingira inahitaji kwa baadhi ya wavuvi kwani mapambanio ya kukabiliana na
mabadiliko ya tabianchi hayanabudi kuongezwa kasi.
Wamesema kuna baadhi ya wavuvi wanashiriki katika vitendo vya uharibifu wa
mazingira kutokana na kutopata elimu ya
kutosha kwani semina za mara moja kila baada ya miezi sita haikidhi mahitaji
Maadhimisho ya siku ya mazingira duniani hapa nchini kitaifa
yanafanyika jijini Mwanza ambapo
hufanyika kila tarehe 5, june duniani
kote.
Mkoa wa Mwanza umechaguliwa kutokana na
changamoto za ukame unaoendelea katika mkoa huo na uharibifu mkubwa wa vyanzo
vya maji kutokana na kilimo kisichoendelevu
na kutumia sumu na makokoro
No comments:
Post a Comment