SERIKALI
kupitia Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeombwa kuingilia kati
ugawaji wa ardhi unaofanywa na viongozi wa kijiji cha Visakazi kilichopo kata ya
Ubena wilayani Bagamoyo mkoani Pwani kabla madhara hayajatokea.
Wakazi
wa kijiji hicho wametoa ombi hilo jana wakati wakizungumza na Mbiu ya maendeleo
ilipotembelea kijijini hapo kwa ajili ya kuzungumza na viongozi pamoja na
wananchi juu ya zoezi hilo la ugawaji wa ardhi ambalo limekuwa likilalamikiwa
na wananchi hao.
Wanakijiji
hao akiwemo bwana Athuman Mgama na Samuel Anatory wamewatupia lawama viongozi
wa kijiji kwa madai kwamba wamekuwa wakigawa ardhi yao kwa wafugaji jamii ya
wamasai bila ya kuwashirikisha wananchi hali inayotishia kuzuka kwa mgogoro
baina ya wafugaji na wakulima.
Kwa
upande wao baadhi ya Viongozi wa Kijiji hicho ambao ni Bi Halima Omari na Bwana
Paulo Mtinange wamekiri kuwepo kwa mgogoro huo lakini wamekana kuhusika nao
kama wanavyodai wananchi.
Kwa
mujibu wa wanakijiji hao,mgogoro huo ni wa muda mrefu na kila kiongozi ajaye
katika kijiji hicho amekuwa akiuongeza badala ya kuutafutia ufumbuzi kabla
haujaleta madhara kama ilivyo kwa maeneo mengine.
No comments:
Post a Comment