Saturday, May 31, 2014

Ban Ki Moon asifu jitihada za Raisi Jkaya Kikwete na mchango wake katika kupigania afya ya mama na mtoto



KATIBU  Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki Moon,amesifu jitihada za Rais Jakaya Mrisho Kikwete na  mchango wake mkubwa katika kupigania Afya ya Mama na Mtoto.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Muandishi wa Habari wa rais msaidizi bwana Premi Kibanga,Bw. Ki Moon ametoa pongezi hizo jana  wakati alipokuwa akizungumzia  juhudi za kumuokoa Mama na Mtoto ikiwa ni  mwishoni mwa mkutano wa siku 3 kuhusu Afya ya Mama na Mtoto uliofanyika nchini Canada.

 
Rais Kikwete na Waziri Mkuu wa Canada Bw. Stephen Harper, kwa  miaka minne  wamekuwa Wenyeviti Wenza wa Kamisheni ya Habari na Uwajibikaji katika masuala ya Afya ya Mama na Mtoto , ambayo imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha vifo vya Watoto wachanga na Mama wajawazito vinapunguzwa  kwa nusu ifikapo Mwaka 2015.

Pamoja na mafanikio hayo, Rais Kikwete amesema bado jitihada zinahitajika katika kuhakikisha mafanikio hayo yanaimarishwa zaidi na kwamba hayapotei .

Aidha Rais Kikwete amesema Tanzania inahitaji vitega uchumi zaidi kutoka Canada na hivyo kuwakaribisha wawekezaji na wafanyabiashara wa Canada kuja kuwekeza Tanzania.

Rais Kikwete anatarajia kuondoka Toronto nchini Canada  kurejea Dar es Salaam, kupitia Marekani.


No comments:

Post a Comment