MKUU wa wilaya
kilosa,mkoani Morogoro Elias Tarimo
ametoa wito kwa madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Kilosa kusimamia maendeleo ya taaluma shuleni kwa
kufuatilia utoro wa walimu kama wanaingia madarasani kufundisha na wanafunzi kama wanahudhuria madarasani .
Wito huo ameutoa hivi karibuni
katika kikao cha madiwani kilichofanyika mjini hapo kilichokutanisha madiwani
wote wa halmashauri ya wilaya , watendaji kata na wataalamu wa halmashauri ya
wilaya
.
Tarimo amesema kuwa wilaya ya kilosa
imekuwa na changamoto ya elimu kutokana na kushuka kwa kiwango cha elimu
ambapo mwaka 2013 kiwango kilishuka kutokana na ufaulu wa wanafunzi kufikia
asilimia 38 tu.
Ameelza kuwa madiwani wanapaswa kusimamia
utekelezaji wa kiwango cha taaluma
shuleni kwani wakati nwingine walimu hawawajibiki ipasavyo kwa kuingia
madarasani kwa kufundisha watoto ambapo pia watoto wamekuwa watoro shuleni mitaani
kuuza biashara na kuchunga mifugo.
No comments:
Post a Comment