WAKAZI wawili
ambao ni ndugu jamii ya kimasai Sepuka Koliji mwenye umri wa miaka (29) na Mogela Koliji mwenye umri wa miaka (20) wakazi wa
kijiji cha parakuyo tarafa ya Kimamba wilayani Kilosa,mkoa
wa Morogoro wanashikiliwa na jeshi la
polisi wilayani humu kwa kosa la wizi wa mifugo.
Akizungumza
na mbiu ya maendeleo kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Leonard Paulo amesema
kuwa tukio hilo limetokea mapema mwezi huu huko maeneo ya kijiji cha parakuyo
wilayani hapa.
Kamanda PAULO amesema kuwa siku ya tukio watuhumiwa hao
ambao ni ndugu kwa pamoja waliiba ng’ombe wapatao 21 ambao ni mali ya
ndugu yao ajulikanae kwa jina la Kisonga Koliji ambapo walikutwa wakiwapeleka
mnadani maeneo ya melela kwa ajili ya kuwauza
No comments:
Post a Comment