DIWANI wa kata ya Masanze wilaya ya Kilosa,mkoani Morogoro Mheshimiwa Jonathan
Kambikiye amewataka watendaji wa vijiji kwenye kata hiyo kusimamia
masuala ya usafi ili kuepuka magonjwa mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa homa
ya Dengi ulioibuka hivi karibuni katika
mikoa mbalimbali nchini.
Akizungumza
na Mbiu ya Maendeleo mapema leo mjini Kilosa mheshimiwa Kambikiye amesema,
watendaji wa vijiji wanawajibu wa kuhakikisha kuwa suala la usafi kwenye kata hiyo linapewa kipaumbele.
Amesema
kuwa suala la usafi ni muhimu katika kata hiyo na wahakikishe wananchimba vyoo , kwa kila kaya
sanjari na kuchimba mashimo ya taka na
kufyeka sehemu zenye vichaka.
Mbali
na hayo diwani huyo ametoa wito kwa
wataalamu kwenye kata hiyo kutoa ushauri na kushirikiana na watendaji wa kata
na vijiji kuhakikisha wanakusanya mapato ya vijiji ipasavyo itakayosaidia
kuleta maendeleo kwenye kata hiyo.
No comments:
Post a Comment