Friday, May 30, 2014

KIWANGO cha unywaji wa maziwa kwa watanzani bado ni kidogo sana, ikilinganishwa na kile kilichopendekezwa na shirika la chakula na Afya duniani.



MAADHIMISHO ya 17 ya wiki ya Maziwa  kitaifa yamezinduliwa leo mkoani Mara ambapo imeelezwa  kuwa kiwango cha unywaji Maziwa bado ni kidogo ikilinganishwa na kile kilichopendekezwa na Shirika la Chakula na Afya Duniani.

Mwakilishi wa Kaimu Mkuu wa mkoa wa Mara Bw Jackson Msome ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Musoma ameyasema hayo katika uzinduzi wa maadhimisho ya 17 ya wiki ya Maziwa katika uwanja wa Shule Msingi Mukendo Manispaa ya Musoma mkoani Mara.
 

Amesema lengo la Maadhimisho hayo ni kulenga shughuli za wadau wa Maziwa ingawa kuna changamoto kubwa kwa viwanda vya usindikaji Maziwa nchini huku akisema kuwa kutokana na uzalishaji kwa sasa wastani wa unywaji Maziwa kwa mtu  ni lita 45 kwa mwaka  huku viwango vilivyopendekezwa na Shirika la WHO na FAO ni kunywa Maziwa lita 200 kwa mwaka. 

Katika Maadhimisho hayo ambayo kilele chake ni june mosi mwaka huu shirika la taifa la hifadhi ya Jamii NSSF  limeendesha kambi ya upimaji wa afya bure kwa wakazi wa Mkoa wa Mara ambapo litaendesha zoezi hilo kwa siku tatu na baadae kuelekea katika mikoa ya shinyanga, Geita na  Kagera





















No comments:

Post a Comment