![]() |
| Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk Rajabu Rutengwe |
KUNDI la watu zaidi ya wanakijiji 60 wa kijiji cha Mabana wilayani
Kilosa wametua ofisini kwa mkuu wa mkoa Morogoro Dk.Rajabu Rutengwe na mwili wa
Mkulima Said Madule (76) aliyeuwawa shambani kwake na wafugaji jamii ya Masai
ili ashuhudie na kusadiki kuwa kumekuwa kukitokea maafa kila inapotokea msimu
wa kilimo mashambani.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti
ofisini hapo baadhi ya wanakijiji hao na wanafamilia walisema wameamua kufanya
hivyo ili kumsadikisha mkuu wa mkoa huo,mkuu wa polisi na usalama kuwa jamii
hiyo inanguvu ya kufabnya lolote kwa wakulima bila serikali kuchukua hatua
zozote za kisheria.
"tumelia sana,tumesema sana
lakini hayo yote yamepuuzwa na viongozi wote kuanzia wa vyama vya siasa ngazi
zote hadi wa serikali ngazi zote hapa mkoani...hasa jeshi la polisi wilayani kwetu
tunadiriki kusema limemezwa na wafugaji kwa asilimia zote" alisema Masudi
Mohamedi (76)
Wakionyesha kuchoshwa na utendaji wa
jeshi hilo kuanzia kituo kidogo kilichopo Dumila hadi wilaya hiyo ya Kilosa
walisema tarehe 17. Januari Marehemu Mzee Said alikwenda shambabni kwake
kutazama mazao yake ya Tikiti ambapo alikuta kundi la Ng'ombe waliotajwa kuwa
mali ya mfugaji aliyetambulika kwa jina la Leteo.
Walisema alipojaribu kuwaondoa
shambani humo,ghafula alivamiwa na wafugaji hao kisha kumjeruhi kichwani karibu
na kosogo na sime kisha kutoweka baada ya mzee huyo kupoteza fahamu na kuanguka
chini ambapo aliokotwa na shemeji yake Tabu Ambuje(65).
Katika tukio hilo wanakijiji
walifanikiwa kukamata kundi la Ng'ombe waliokuwa shambani humo kisha kuwahifazi
ofisi ya mtendaji kijiji sambamba na mmilikiwake aliyetajwa kwa jina la Leteo
aliyefikishwa polisi kituo cha Dumila ili ashikiliwe hadi hali ya mgonjwa
itakapokuwa nzuri
Tofauti na walivyodhani na kuelewa
mfugaji huyo aliachiwa siku hiyo hiyo na kuja kuchukua Ng'ombe hao kwa kulipa
kwa mtendaji wa kijiji hicho cha Mabana faini ya shilingi 150,000, walipouliza
kituoni kulikoni aachiwe mtuhumiwa aachiwe ilihali mgonjwa hali yake ni mbaya
walijibiwa wajali kuuguza mambo ya polisi hayawahusu.
Mbali na majibu hayo kituo kidogo
cha polisi Dumila,pia walipojarubu kupata ufafanuzi juu ya taratibu za dhamana
kwa mtuhumiwa aliyejeruhi polisili wilayani Kilosa,walijibiwa kuwa jukumu lao
ni kuzika kama hawataki wakae na maiti hadi atoe harufu ndio wazike.
Hata hivyo juhudi za kuonana na mkuu
wa mkoa huyo zilishindikana na kushauriwa na badhi ya walinzi ofisini hapo
kwenda kwa kamanda wa polisi mkoa kwakuwa ni mkuu wa ulinzi na usalama mkoani
humo.
Kufuatia mjadala huo wa mda mrefu
kamanda wa polisi mkoani Morogoro Leonard Paul alikwenda kijijini Mabana na
kuwaeleza wananchi msibani kuwa jeshi linakili kuwepo uzembe katika utendaji
nakuwa mara moja litachukua hatua kali dhiidi ya wahusika wote juu ya afa hilo
na mengine yatakayotokea.

No comments:
Post a Comment