Tuesday, June 3, 2014

MAZISHI ya mtoto aliyekaa kwenye boksi kwa miaka mitatu yafanyika Moro leo


LAANA na maagizo mazito kwa vyombo vya dola dhidi wazazi na walezi wa Mtoto marehemu Nasra Rashidi(4) yametolewa  leo na viongozi wa serikali na dini Mkoani Morogoro wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa mtoto huyo uwanja wa Jamuhuri.  

Katika salamu za mkoa kwa mamia ya watu uwanjani hapo mbele ya jeneza lililokuwa na mwili wa marehemu Nasra,Mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera aliiomba Mahakama na jeshi la polisi mkoani humo kutokuwa na huruma na wazazi hao.

"bila kutafuna maneno,huruma wala haya kwa yeyote hapa ukatili huu uliomfungulia pepo mtoto huyu baada ya kufanyiwa ukatili,fedheha kwa mkoa na Taifa dhambi hii iwatafune kuanzia sasa hapa hapa duniani na hata baadae mbinguni"alisema Bendera akionyesha kububjikwa machozi.

Katika salamu hizo mkuu huyo alisema haiingii akilini kwa mtoto mwenye baba,mama ndugu na jamaa wachamungu kupitia dini fulani duniani akafichwa na kuteswa kwenye boksi kwa zaidi ya miaka mitatu kwa sababu ya aina yoyote iliyopo hapa duniani halafu akafurahiwa.  

"jamani tumuogope mungu na kumtii Mungu, haifurahishi wala haifai hata kusimulia nawaomba Mahakama mkishirikiana na polisi upelelezi hawa ambao hata dhamana wamekosa wateseke kama alivyo teseka mtoto Nasra"aliongeza


Kwa upande wa mbunge wa jimbo la Morogoro Abdulahzizi Abood  alisema msiba wa Nasra umekuwa gumzo katika vikao vya Bunge vinavyoendelea mjini Dodoma na kuamsha fedheha nyingine kwa taifa ukiuonyesha mkoa kutokuwa na huruma ya ukatili kwa watoto.

"kama kuna wengine wanafanya hivi binafsi nawasihi waache na kama hawawataki watoto hao wawalete tuwatafutie watu wa kuwale,nin aimani wapo wanatafuta watoto"alifafanua Abood.

Akihitimisha maombolezo uwanjani hapo Shekhe wa Morogoro Ally Omari alisema mateso ya mtoto huyo hayawezi kutenganishwa na ushirikina kwakuwa wazazi na walezi walilifahamu jabo hilo na kuendelea na shuguli zao ikiwemo sokoni na mama lishe.

Akionyesha kukerwa na mtoto huyo kufanywa 'Ndondocha' Shekhe Omari alisema wazazi wa sasa wakiwemo wa Marehemu Nasra wanalaa zinaa 'Michepuko' ambayo mwisho wake ni aibu kama iliyojitokeza katika msiba huo.

No comments:

Post a Comment