WAKATI tukielekea
kuadhimisha siku ya mazingira duniani ambayo
hufanyika juni 5, kila mwaka wakulima wa kilimo cha umwagiliaji Msosa
wilayani Kilolo mkoani Iringa wameiomba ofisi ya makamu wa Raisi kitengo cha
mazingira kuongeza kasi ya utoaji wa elimu ya uhifadhi wa mazingira kwa wakulima wadogo wadogo
.
Wakiongea na mbiu ya maendeleo
mapema jana katika vijiji vya Mtandika na Msosa wilayani humo . wakulima hao
wamesema kuwa mabadiliko ya tabia nchi
yanakuja kwa kasi sana na ndio maana kuna mambo yanatokea kila uchao na uchwao
hivyo ni vyema wakulima wakaelimishwa
mbinu mbadala ya kukabiliana na hali hiyo.
Wamesema wao, wanatumia mbolea za
viwandani katika kuzalisha mazao mbalimbali ukizingatia tunatumia kilimo cha
umwagiliaji ambacho kina hitaji wataalamu wa masuala ya mazingira kabla ya
utekelezaji wake, lakini kutokana namchakmchaka wa mapambano ya umaskini
kupitia sekta hiyo sanjari na uhaba wa wataalamu wa mazingira ngazi ya wilaya,
sehemu kubwa tunalima kienyeji zaidi.
Bwawa la Mtera lililopo kijiji cha Mkungugu, tarafa ya Ismani ,mkoani Iringa ambalo hutumiwa kwa kilimo cha umwagiliaji katika vijiji vinavyozunguka bwawa hilo
No comments:
Post a Comment