Tuesday, June 3, 2014

UHABA wa wataalamu wa mazingira unachangia kukithiri kwa uchafu katika masokoni moja


UHABA  wa vifaa vya kisasa na wataalamu wa mazingira ni miongoni mwa  ni mambo yanayochangia kukithiri kwa uchafu katika masoko mengi jijini Dar es salaam. IMEELEZWA

Wafanyabiashara wa nazi katika soko la Ilala, jijini Dar es salaam wameeleza    hayo leo katika mahojiano  maalum na mbiu ya maendeleo.

Wamesema wafanyabiashara wengi wanalipa ushuru wa soko kama unavyohitajika lakini mara nyingi majiibu ya uongozi  ni kukosekana kwa wataalamu wa kutosha wa masuala ya mazingira katika soko hilo sanjari na uhaba wa vifaa.

Hata hivyo wametaka mamlaka husika kutafuta mzizi wa matatizo hayo kwani hali ya soko hiklo kiafya ni mbaya sana kutokana na bidhaa nyingi kupangwa chini hali inayotishia usalama wa mlaji kiafya.

No comments:

Post a Comment