Thursday, September 4, 2014

FIFA yatishia kuiondoa Nigeria


SHIRIKISHO  la soka ulimwenguni FIFA limetishia kutimua Nigeria kutoka kwa shirikisho hilo iwapo Chris Giwa hataacha kujidai kuwa rais wa shirikisho la soka nchini humo.

Shirikisho hilo limesema Nigeria ina hadi Jumatatu kubadili mambo kwani halimtambui bwana Giwa kama Rais wa shirikisho la soka nchini humo.
Ikiwa shirikisho hilo litawekewa marufuku, marufuku hiyo itaondolewa tu iwapo bodi halali iliyoishidhishwa kushika uongozi , Aminu Maigari akiwa rais wake, itaruhusiwa kuendelea na kazi zake.
Uchaguzi mpya utahitajika kufanywa haraka iwezekanavyo.
Siku ya mwisho kwa Giwa kujiondoa kama rais wa NFF ilifikiwa na FIFA Jumatano. Hii ni baada ya Giwa kukosa kutii makatibu

No comments:

Post a Comment