Saturday, April 4, 2015

MBUNGE agundua Ufisadi wa milioni 700


Mbunge wa Morogoro (mwenye fulana nyekundu)akiwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na makazi Mheshimwa Williamu Lukuvi mjini Morogoro
MBUNGE wa Jimbo la Morogoro mjini Abdulaziz Abood amevumbua ufisadi wa shilingi Mil.700 unaodaiwa kufanywa kwa siri baina ya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na kampuni ya ujenzi ya China ijulikanayo kwa jina la GROUP SIX LTD kwenye ujenzi wa Standi kuu ya mabasi ya mikoani na nje ya nchi Msamvu.


Uvumbuzi huo alioupata juzi kwenye ziara ya kushitukiza stendi hapo ulidhihilika baada ya kumtaka mhandisi wa manispaa hiyo Ndelembi Sangija aliyeambatana nae kukataa kumwonyesha mbunge huyo mikataba waliyoingia na kampuni hiyo akidai hadi uongozi wa manispaa utakaporidhia.

"ok basi naomba nionyeshe hata ramani ya mradi huu na nieleze mgawo wa hawa Mamalishe katika hivi banda utakuje...siombi kama Abood ila kama mwakilishi wa wananchi kwenye vikao vya maamuzi" alifafanua Abood ambae hata hivyo hakuonyeshwa.

Mbele ya viongozi wa chama  cha mapinduzi,diwani wa Kata ya Mafisa Francis Kayenzi na waandishi wa habari kwenye kikao alichoitisha kupata taarifa sahihi za mradi huo mbunge huyo alielezwa kuwa mikataba hiyo nisiri na hapaswi kuijua hadi uopngozi utakapo ridhia.

"unajua inashangaza na sijui kwa nini uongozi wa manispaa haujaitikia mwito wangu kuja hapa kama taarifa wanazo kwa muda mrefu tena kwa maandishi...sasa hata tukitaka kuomba fedha seriakli nitafanyaje wakati sina taarifa juu ya uwepo wa mradi huu"alina kuongeza.

"inashangaza kwa halmashauri ilishalipa zaidi ya shilingi Mil. 700 kununua ardhi kwa ajili ya  kupanua eneo utekelezaji wa  mradi huo kituo cha mabasi msamvu wakati manispaa inamaeneo mengine mbadala.

Kwa upande Injinia Sangija akitoa ufafanuzi wa kushindwa kuionesha ramani mbele ya Mbunge huyo alisema  mpaka aonane na uongozi wa Halmshauri  hiyo na kumruhusu kuzikabidhi nyaraka hizo ikiwemo ramani kwa mbunge huyo .



No comments:

Post a Comment