Monday, July 4, 2016

WANAWAKE Pemba washauriwa kutumia kilimo mbadala ili kukabiliana na changamoto za kipato

Wakulima wa Pemba, Zanzibar wakiwa shambani 
KILIMO mbadala ndiyo njia pekee ya kukabiliana na changamoto za umaskini wa kipato kwa wanawake, imefahamika.

Hayo yamebainishwa hivi karibuni na wanakikundi wa Pemba Community Forest katika mazungumzo yao na wanahabari

Wanawake hao wa wanasema ‘’Jamii zetu wanatumia mbinu bora ya kulima bustani ndogo inayozidisha upatikanaji wa matunda na mbogomboga kwa afya bora”.
Wamefafanua kuwa ni muhimu kwa jamii kuwekeza katika kilimo cha bustani na mbogamboga ili kukuza uchumi , kuhifadhi mazingira sanjari na kupambana na magonjwa yanayosabishwa na lishe duni.


No comments:

Post a Comment