Saturday, October 29, 2016

WORLD vISION yatumia shilingi bilioni 2 kuondoa watoto mitaani watoto 1,323



SHIRIKA la kimataifa lisilo la kiserikali la ‘World Vision’ lenye makao yake makuu la Australia  likishirikiana na mashirika sita yasiyo ya kiserikali nchini limetumia Dola za kimarekani 960,103 sawa na zaidi ya shilingi Bil.2 kuondoa mitaani zaidi ya watoto 1,323 na kuwakwamua kiuchumi zaidi ya wazazi na walezi 1,240 Manispaa ya Morogoro.


Hayo yamo kwenye risala mbele ya mkuu wa wilaya ya Morogoro aliyewakishwa na afisa Maendeleo ya jamii Manispaa hiyo Joycerebeka Paul katika hafla ya uhitimishaji mradi wa kuondoa watoto mitaani na kuinua kiuchumi familia masikini ujulikanao‘Hope Street Chidren’.

Katika risala hiyo ya meneja mradi Evans Rwamuhuru iliyosomwa na afisa utawala wa shirika la Faraja Jayna Mfinanga,kiasi hicho cha fedha kimewezesha kuondoa idadi hiyo ya watoto wakiwemo waliokuwa hatarini kukuingia makundi ikiwemo kufanyishwa kazi kulipwa ujira mdogo kwa muda na kutwa kwa kuwapatia elimu ya msingi na ufundi.
“ili kufanikisha na kuyafanya maelengo yetu kuwa endelevu mradi umeto mafunzo kwa zaidi ya watu 1,240 kwa kutoa elimu na kuanzisha vikundi 35 vya ujasiliamali ambavyo sasa vina hisa shilingi Mil.386,mikopo yenye thamani ya shilingi Mil.320 na kujikusanyia shilingi Mil.58 kwa ajili ya mfuko wa jamii na watoto…ukweli tumewakwamua katika hatua ya kwanza”alisoma Jayna.
Alitaja mashirika yaliyoshirikiana na World Vision kufanikisha mradi huo kuwa ni pamoja na Faraja Trust Fund,Neema resource Foundation,Morogoro paralegal centre,Mission to the Homeless centre,Hakuna matata charity Organization Save Family Tanzania charity, na Emerge Tanzania.
Akisoma risala ya watoto,mtoto Fredrick Lyiobha alilia serikali akiitaka kuwaangalia watoto kwa jicho la pekee ikizinagtiwa kuwa huenda wakakosa msaada baada ya mradi kuisha hivyo kuwalazimu kurudi mitaani kama ilivyokuwa awali.
“Ndugu Mkuu wa wilaya sisi ni watoto tunaoendelea kuhitaji msaada wa hali na mali katika kujikwamua na chanagamoto za maisha ya kilasiku…tunaililia seriakali kutuendeleza kuanzia hapa tulipo ili tukie ndoto.






No comments:

Post a Comment