Tuesday, April 29, 2014

CHAMA cha wakulima yaisimamisha bodi ya chama kwa kufanya kazi kwa hasara



MKUTANO  mkuu wa Chama cha wakulima wa Tanganyika (TFA)umelazimika kuisimamisha bodi ya chama hicho, baada ya wajumbe wa kamati ya uchunguzi kukamilisha kazi yake  kuhusu sababu inayopelekea chama hicho  kuendelea kupata hasara .

Wakiongea katika mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika  jijini  Arusha juzi,wajumbe wa mkutano huo  wamekubaliana kwa kauli  moja kuisimamisha bodi  ya chama hicho,na kuipa nafasi hiyo kamati ya uchunguzi isimamie kwa muda, hadi chama hicho  kitakapounda bodi mpya.

Wajumbe hao wamesema, baada ya kamati  kufanya uchunguzi wa kina imebaini kuwa, uongozi wa bodi iliyokuwepo madarakani haukuwa na  uwezo wa kukiendesha chama hicho , wala kubuni miradi ya maendeleo hivyo ni bora wachaguliwe viongozi wengine wenye uwezo wa kuifanya kazi hiyo.

Kufuatia hali hiyo ,mwenyekiti wa kamati  ya uchunguzi Bw Maynard Swai ,na Mwenyekiti  wa muda wa mkutano huo Bw Ali Mwamba ,wamewashauri wajumbe wa mkutano huo  kuwa makini katika uchaguzi ujao ,ili waweze kupata  viongozi waadilifu na wenye uwezo kiutendaji na  kukiongoza  chama hicho kikongwe hapa nchini.

No comments:

Post a Comment