Tuesday, April 29, 2014

BAADHI ya mila na desturi nchini zinachangia kuduma kwa watoto chini ya miaka mitano



IMEELEZWA kuwa baadhi ya mila na desturi za makabila nchini zinachangia kuongezeka kwa tatizo la utapiamlo na kudumaa kwa watoto chini ya watoto chini ya miaka mitano nchini.

Wataalamu toka Taasisi ya lishe nchini wambainisha hayo mapema leo katika mahojiano maalum na Mbiu ya Maendeleo viwanja vya mnazi mmoja kuhusu hali ya lishe nchini.

Wamesema tafiti zilizofanywa mwaka 2010 kuhusu hali ya lishe  zinaonesha hali ya Udumavu kwa watoto chini ya miaka mitano kwa  baadhi ya mikoa ni ya juu kutokana na mila na desturi katika suala la vyakula na lishe.

Watalaamu hao wamefafanua kuwa, mkoa wa Dodoma unaongoza kiwango cha udumavu kwa asilimia 56 ukifuatiwa na Lindi asilimia 52 ambapo mkoa wa Kilimanjaro una asilimai 28 ikiwa ni asilimia ndogo, ukifuatiwa na mkoa wa Mara wenye  asilimia 31 ya Udumavu  wa watoto chini ya miaka mitano nchini.
  




No comments:

Post a Comment