WAFANYAKAZI wa Wizara ya Fedha wameaswa
kufanyakazi kwa bidii na kujituma kwa moyo kwa lengo la kukuza uchumi wa nchi
ili taifa liweze kusonga mbele na kufikia malengo yake.
Kauli
hiyo imetolewa na Waziri wa Fedha Mheshimiwa Saada Mkuya Salum wakati wa
kufungua mkutano wa Baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo hivi karibuni jijini
Dar es salaam.
Katika
mkutano huo, Waziri Saada aliwapongeza wafanyakazi hao kwa kufuata maelekezo ya
kuwa na vikao vya baraza la wafanyakazi mara mbili kwa mwaka kulingana na
mkataba ambapo lengo la mkutano huo ni kupata taarifa ya utekelezaji wa bajeti
ya mwaka 2013/14 pamoja na kupitia na kujadili bajeti ya mwaka 2014/2015.
Mkutano
wa baraza hilo umefanyika kwa kuzingatia agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete na katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue wa
kuitisha vikao kulingana na utaratibu uliowekwa.
No comments:
Post a Comment