WIZARA za ujenzi na
uchukuzi zimepewa changamoto ya kuhakikisha zinatafuta ufumbuzi wa kudumu wa
matatizo ya kuharibika kwa madaraja ya njia ya reli katika maeneo ya Kilosa ,
Mzaganza na Godegode ili kuwawezesha wananchi wanaotumia usafiri wa reli kuonddoa
na adha ya mara kwa mara hasa kipindi cha masika.
Wakiongea na mbiu ya maendeleo hivi
karibuni katika wilayani Mpwapwa, mkoa wa Dodoma wakulima wa alizeti, mpunga ,
maharage na vitunguu wa vijiji vya Lumuma,Pwaga, na Kibakwe wamesema kuwa huwa
wanapata wakati mgumu katika kipindi cha masika kila mwaka kusafirisha bidhaa zao mbalimbali kwani
ndio usafiri wanaoutegemea kwa asilimia zaidi
ya 70.
Wamesema ,shughuli nyingi za
kiucghumi kati ya mkoa wa Morogoro na Dodoma kupitia Kilosa kwa sasa zinasuasua
kwa kutumia usafiri wa reli na magari kwani hali ya miundo mbinu ya reli na
barabara ni mbaya kiasi chakutopitika.
Tumekuwa tukitumia njia ya reli
kusafirisha bidhaa na malighafi mbalimbali za kilimo kwaajili ya shughuli za
uchumi na kijamii kwenda Kilosa kupitia
vijiji vya Kitati , Kidete na
Lumuma kwa njia ya reli na barabara , lakini kwasasa inatulazimu kutumia njia
ndefu ya kuzunguka kupitia Mpwapwa mjini hali ambayo ni gharama kubwa.
No comments:
Post a Comment