ZAIDI ya kaya 100 katika kijiji cha
Mcharo na Kiwasi wilayani Bunda Mkoani Mara zinakabiliwa na uhaba wa chakula
baada ya mihogo waliyokuwa wamelima kukumbwa na ugonjwa wa batobato,michilizi
kahawia,ukame wa muda mrefu kwa mazao ya mahindi pamoja na ardhi inayotumika
kwa shughuli za kilimo kukosa rutuba.
Imeelezwa
kuwa kaya hizo ni zile ambazo zinazokaliwa na wazee wasiojiweza, wajane,
wagane, akinamama na watoto ambazo sasa zimeingizwa katika mpango wa kunusuru
kaya maskini na zilizo katika mazingira hatarishi unaotekelezwa na mfuko wa
maendeleo ya jamii tasaf awamu ya tatu uliopo chini ya ofisi ya rais.
Kwa
Upande wake Mkurugenzi wa fedha wa mfuko wa maendeleo ya jamii Tasaf bwana
Isaya Wambura akizungumza na wakazi wa kijiji cha Mcharo katika Mkutano
uliohudhuriwa na afisa mkaguzi mwandamizi wa benki ya dunia pamoja na
mchumi mwandamizi wa shirika la maendeleo la umoja wa mataifa ( UNDP ) amesema
kila baada ya miezi miwili tasaf itawasilisha shilingi 34,000 kwa kila kaya,
kiasi ambacho kinalalamikiwa na baadhi ya walengwa kwamba hakitoshelezi kukidhi
mahitaji kutokana na baadhi yao kuwa na familia za watu zaidi ya wanane.
No comments:
Post a Comment