TAASISI
ya Karibu Tanzania Association (KTA)inayojishuhurisha na utoaji wa Elimu kwa
watu wazima pamoja na kuendeleza vyuo vya maendeleo ya wananchi nchini
imedhamiria kuwasaidia wasichana wanaokatisha masomo kutokana na
ujauzito.
Kauli hiyo
imetolewa leo mjini Morogoro na Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Bwana George Mangoma
wakati wa ufunguzi wa Warsha ya siku tatu pamoja na mkutano mkuu wa mwaka ambao
utakwenda sambamba na uchaguziwa viongozi wa taasisi hiyo.
Bwana
Mangoma amesema kuwa moja ya majukumu ya taasisi hiyo ni kukuza maendeleo
ikiwemo mkakati huo wa kuwasaidia wasichana ambao wengi wao hukumbana na
changamoto nyingi pindi wanapopata ujauzito wakati wakiwa shule.
Taasisi
hiyo ya KTA ambayo inajumuisha vyuo 55 vya maendeleo ya jamii
ilianza kufanya kazi zake hapa nchini tangu mwaka 1990 na imekua ikishiriana
kwa ukaribu na Taasisi ya Kimataifa ya Karibu Sweden Association(KSA)
No comments:
Post a Comment