MVUA zinazoendelea kunyesha
katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo mkoani Morogoro zimesababisha uharibifu
wa miundo mbinu,hali iliyowalazimu wananchi wanaotumia barabara ya Ulanga hadi
Ifakara kushirikiana na madereva kuchimba barabara kunusuru magari
yaliyokwama njiani ili yaweze kuendelea na safari,huku wengine wakilazimika
kulala njiani kutokana na ubovu huo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Mbiu ya
maendeleo hivi karibuni,baadhi ya abiria hao wameiomba serikali kufanya
jitihada za makusudi kujenga sehemu korofi za barabara ya ULANGA-IFAKARA kwa
kiwango cha lami, ili kukabiliana na changamoto hiyo ya ubovu wa barabara, hasa
wakati wa mvua.
Mvua zinazoendelea kunyesha
zimesababisha mafuriko katika wilaya ya Kilombero, ambapo makalavati
yaliyopo Ifakara katika barababara ya kuelekea Ulanga kabla ya kivuko,
yamezolewa na maji, huku baadhi ya nyumba zikijaa maji na nyingine kubomoka
kabisa.
No comments:
Post a Comment