Sunday, April 27, 2014

WAKULIMA wilayani Kilosa watakiwa kutumia mafunzo ili kuongeza mavuno na tija



WAKULIMA wadogo  wilayani KILOSA waliopatiwa mafunzo ya kurutubisha udongo kwa kutumia njia mbalimbali za kuongeza virutubisho katika udongo kupitia MRADI uliopo chini ya SHIRIKA la  farmradio International unaofadhiliwa na FAIDA MALI pamoja na Jukwaa la Mapinduzi ya Kijani Afrika AGRA  wametakiwa kuendeleza  elimu hiyo ili kupata mavuno bora na yenye  tija

Hayo yameelezwa juzi na Afisa vipindi vya redio kutoka AGRA Bwana Qureish Noordin alipowatembelea wakulima hao katika shamba darasa ambapo amewakumbusha kutumia mbinu bora za kilimo walizofundishwa sambamba na kutumia mbolea katika ukuzaji wa mimea.

Bwana Qureish amesema wakulima wengi wamekuwa na tabia ya kutotumia mbolea wakidai udongo wa ardhi wanayoitumia una rutuba na mbolea zinaharibu ardhi  mtazamo ambao  unaipotosha jamii na kurudisha nyuma maendeleo katika kilimo.
  

Mradi wa kurutubisha udongo kwa kutumia njia mbalimbali za kuongeza virutubisho katika udongo ni mradi wa miaka miwili na ulianza mwaka jana ukiwa na lengo la kutoa elimu kwa wakulima katika kulima kilimo chenye tija  na kuongezea kipato cha mkulima wilayani Kilosa.



No comments:

Post a Comment