UONGOZI wa
Kijiji cha Lusanga kata ya Diongoya Tarafa ya Turiani Wilayani Mvomero
mkoani Morogoro umesema unaendelea na jitahada za kutatua mgogoro wa
ardhi uliopo baina ya wananchi wa kijiji hicho pamoja na uongozi wa shule ya
sekondari Lusanga.
Kauli hiyo
imetolewa juzi katika sherehe za mahafali ya pili ya kidato cha
sita yaliyofanyika shuleni hapo na Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bwana Hussen
Mbena wakati alipoombwa kutoa ufafanuzi juu ya uvamizi unaofanywa na baadhi ya
wakazi wa eneo hilo na kusema kuwa mgogoro huo ulikuwepo tangu uongozi
uliopita.
Akisoma
risala katika sherehe hizo mkuu wa shule hiyo bwana Beatus Mwihava amesema
pamoja na mafanikio waliyonayo kitaaluma lakini bado wanakabiliwa na changamoto
kadhaa ikiwemo uchache wa walimu wa masomo ya sayansi pamoja na hesabu huku
akigusia suala la uvamizi wa eneo la shule kuwa ndio tatizo sugu lililopo
shuleni hapo.
.
Jumla ya
wanafunzi 34 wametunukiwa vyeti pamoja na zawadi,wanafunzi hao wanaijiandaa kwa
ajili ya mtihani wao mwisho ambao utafanyika utanyika tarehe tano mwezi wa tano mwaka huu.
No comments:
Post a Comment